JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Walinzi GGM watuhumiwa kwa ujambazi

Kashfa nzito imeukumba Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), baada ya baadhi ya walinzi wake kudaiwa kujihusisha na matukio ya ujambazi wa kutumia silaha.

Imedaiwa kuwa walinzi hao wanapomaliza kufanya matukio hayo yakiwamo ya utekaji na uporaji, fedha zinazopatikana huzitumia kuwaziba midomo baadhi ya viongozi wa vyombo vya dola wasiwafikishe katika mkono wa sheria.

Siri zavuja Bandari

 

*Orodha ndefu ya watumishi aliowaonea Kipande yatajwa
*Wafanyakazi wambatiza ‘Last King of Scotland’ – Idi Amin
*Takukuru yachunguza unyanyasaji huu, malipo mishahara
*Aliyerejeshwa kwa nguvu ya wakubwa apanga kumhamisha
*Mgogoro wazidi kutanuka, amsukia zengwe mshindani kazini
*Yeye, Mwakyembe, wabunge wiki watumia Sh milioni 360
Na Deodatus Balile
Siri nzito zimeanza kuvuja jinsi Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mzee Madeni Kipande (58), anavyofanya unyanyasaji kwa wafanyakazi wa Bandari hiyo, hasa wanawake, vyanzo vimeifahamisha JAMHURI.

Kipande abanwa Bandari

*Nguvu za ajabu alizokuwa nazo zaanza kuyeyuka, alalamika Kikwete hamsaidii
*Marafiki zake wamtaka asimsingizie Rais, wasema amejiharibia mwenyewe
*Ashinikizwa awarejeshe kazini aliowafukuza kibabe, wafanyakazi washangilia
*Aanza kuogopa kivuli chake, ajitolea ‘photocopy’, adai wanaomsaliti anao TPA
*Mtawa asema asihusishwe na Kipande, bandarini wasema JAMHURI mkombozi
*Mwakyembe aweweseka, adai Lowassa, Profesa Tibaijuka hawamtakii mema
Nguvu za ajabu alizokuwa nazo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande (58), zimeanza kuyeyuka kwa kasi baada ya GazetiJAMHURI kuchapisha mfululizo maovu anayotenda kwa kutumia wadhifa wake.

TCAA nako kwafukuta ufisadi

*Wakurugenzi wahariri Waraka wa Hazina

*Mbinu hiyo yawafanya walipane mamilioni

 

Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), inakabiliwa na tuhuma za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Fadhil Manongi, hadi wiki iliyopita bado alikuwa akiendelea na dhima za kiofisi licha ya muda wake wa kung’atuka kuwadia.

Wakati Manongi akijiandaa kuiacha ofisi hiyo, kumekuwa na malalamiko ya matumizi mabaya ya fedha miongoni mwa wakurugenzi ambao ni washirika wake.

Siku za Kipande bandarini zahesabika

*Ni baada ya kuthibitika anatumia vibaya jina la Rais Kikwete, Ikulu

*Amuagiza Mwakyembe amchunguze, wafuatilia kumtukana Balozi

* Mtawa, Gurumo nao wakana, Mwakyembe adaiwa kumwogopa

*Aendelea kukaidi maagizo ya Bodi, amng’oa rasmi aliyeomba kazi yake

Na Deodatus Balile

Siku za Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mzee Madeni Kipande (58), kuendelea kuwa madarakani zinazidi kuyoyoma baada ya Rais Jakaya Kikwete kukerwa na tabia yake ya kutumia jina la Rais kuhalalisha matendo yake yenye kukiuka sheria za utumishi wa umma.

Habari za uhakika kutoka Ikulu na kwa baadhi ya mawaziri waandamizi, zinasema Rais Kikwete baada ya kupata taarifa za Kipande kutumia vibaya jina lake, alichukia na kuamua kumwita Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, na kumpa maagizo mazito.

Hotuba ya Lissu iliyosababisha TBC1 ‘izimwe’

Aprili 12, mwaka huu, Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Tundu Lissu aliwasilisha maoni ya Wajumbe walio wachache katika Kamati Namba Nne kuhusu sura ya kwanza nay a sura ya sita ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wakati akiwasilisha, Televisheni ya Taifa (TBC1) ilikata matangazo yake katika kile kilichotafsiriwa na wengi kuwa ni kuuepusha umma kupata maoni ‘makali’ yaliyomo kwenye hotuba ya Lissu. Kwa kuzingatia haki ya wananchi ya kupata habari, JAMHURI inawaletea hotuba hiyo neno kwa neno. Endelea

UTANGULIZI

Mheshimiwa Mwenyekiti,

Sura ya Kwanza na Sura ya Sita ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (‘Rasimu’) ndizo msingi ambao Rasimu yote imejengwa juu yao. Wakati Sura ya Kwanza inagusa suala la muundo wa Muungano katika ibara moja tu kati ya ibara tisa, Sura yote ya Sita inahusu ‘Muundo wa Jamhuri ya Muungano.’ Suala la Muungano na hasa Muundo wake limetawala mjadala wa kisiasa na kikatiba wa Tanzania kwa zaidi ya miaka thelathini. Ndio maana katika waraka wake wa siri kwa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (‘CCM’), Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ya chama hicho imetamka kwamba “muundo wa Muungano ndiyo moyo wa Rasimu na ndiyo unaoamua ibara nyingine zikae vipi.”

Suala hili pia limetawala mchakato wa Katiba Mpya tangu ulipoanza miaka mitatu iliyopita. Kama alivyosema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Joseph Sinde Warioba wakati wa kuwasilisha Ripoti ya Tume yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar tarehe 30 Disemba, 2013: “Moja ya mambo ambayo yamejadiliwa sana na kwa hisia kali tangu Rasimu ya awali ilipotolewa … ni Muungano wa Tanzania. Jambo kubwa limekuwa juu ya muundo wa Muungano.”

Umuhimu wa suala hili unathibitishwa pia na uamuzi wa Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalum kuelekeza kwamba Kamati zake Namba Moja hadi Kumi na Mbili zianze kujadili Sura ya Kwanza na ya Sita ya Rasimu. Haya ni maoni ya wajumbe walio wachache wa Kamati Namba Nne juu ya Sura hizi mbili.