JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

Hukumu yakosolewa Moshi

Mahakama inadaiwa kupindisha sheria na kumtoza mshitakiwa wa kukutwa na mali ya wizi faini ya Sh 800,000 badala ya kifungo kisichozidi miaka mitatu kama sheria inavyoelekeza.  Mshitakiwa huyo, Devis Kavishe, alikamatwa na gari lililoibwa nchini Kenya mwaka 2012 aina ya…

Sitta akalia kuti kavu

Aliyekuwa Spika wa Bunge la 9 Samuel Sitta wiki iliyopita alipoonyesha nia ya kugombea uspika wa bunge, sasa ameanza kushughulikiwa, JAMHURI limebaini. Duru za uhakika zinasema Sitta anaunda upya mtandao wake ndani ya CCM baada ya mtandao wa awali kusambaratika…

Seif, CUF waanza kuunda Serikali Z’bar

Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amekuwa mwiba mchungu kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar hasa baada ya kutangaza kuwa anasubiri kuitwa na Tume ya Uchaguzi visiwani  humo (ZEC) kumtangaza. JAMHURI lilipowasiliana na Maalim Seif…

Dozi za Magufuli zaanza

Rais Mteule wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli, akiwa anasubiri kuapishwa keshokutwa, tayari ameshaanza kazi zenye mwelekeo wa kuandaa aina ya Serikali atakayoiunda. Habari za uhakika kutoka kwa watu walio karibu na Dk. Magufuli, zinasema amekuwa akitumia muda mrefu…

Uwaziri Mkuu moto

Dk. John Magufuli akitarajiwa kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wiki hii, mjadala wa nani atakuwa Waziri Mkuu na nani atakuwa Spika wa Bunge la Jamhuri, umeshika kasi. Kwa mujibu wa Katiba, mara baada ya kuapishwa Dk. Magufuli atatakiwa…

Polisi wahaha kumlinda Diwani Sandali

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Dar es Salaam, wamekuwa na kibarua kigumu baada ya kuendelea kulinda nyumba ya diwani mteule wa CCM Kata ya Sandali, Abel Tarimo. Tarimo anaelezwa kuwa hapendwi na wananchi, kitendo kinachowafanya watake kuvamia…