Category: Maoni ya Mhariri
Kuna wamachinga wanaovuna mamilioni, walipe kodi stahiki
Hakuna binadamu anayependa kulipa kodi. Lakini Serikali haiwezi kujiendesha bila kodi, hivyo ni wajibu wa kila mtu mwenye sifa za kulipa kodi, kufanya hivyo.
Rais JK, orodha ya mapapa wa mihadarati imeyeyukia wapi?
Katika gazeti hili kuna barua iliyoandikwa na mmoja wa Watanzania walio kwenye magereza Hong Kong, kutokana na usafirishaji mihadarati.
Tanzania inapotea njia
Mwishoni mwa wiki zimetokea habari za kusikitisha. Mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, Said Mohamed Saad, amemwagiwa tindikali usoni na sasa amepelekwa kwenye matibabu nchini Afrika Kusini.
Matusi kwa Rais wetu hayakubaliki
Kwa muda sasa, kumekuwapo maneno mengi kutoka kwa Rais Paul Kagame wa Rwanda yakimlenga Rais wetu, Jakaya Kikwete. Chanzo cha yote haya ni mapendekezo ya Rais Kikwete ya kumwomba Rais Kagame aketi na waasi wa kundi la FNBL ili kukomesha mapigano na mauaji yanayoendelea Rwanda na upande wa mashariki kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Iddi Simba lazima ashitakiwe upya
Ugeni mkubwa uliofika hapa nchini umeshaondoka. Ugeni huo ni wa Rais Barack Obama wa Marekani, Rais mstafu George W. Bush wa Marekani, marais zaidi ya 10 kutoka mataifa mbalimbali Afrika na duniani kwa jumla, pamoja na mawaziri waandamizi kutoka mataifa mbalimbali.
Saruji kutoka nje ya nchi isizuiliwe
Wiki iliyopita baadhi ya wamiliki wa viwanda vya kuzalisha saruji wamekaririwa na vyombo vya habari wakidai kuwa wanataka saruji kutoka nje ya nchi izuiliwe kuingia hapa nchini. Wanajenga hoja kuwa saruji kutoka nje itaua viwanda vya ndani.