JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Halmashauri ya Geita yatafunwa

* Sh mil 763.8 zakwapuliwa kifisadi

* Mwenyekiti CCM Mkoa ahusishwa

* Waandishi wa habari wapata mgawo

Siku chache baada ya gazeti hili kuchapisha taarifa za nyaraka zinazoonesha Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilipokea Sh bilioni 11.1 za kununua madawati lakini fedha hizo hazijulikani zilivyotumika, taarifa nyingine zimepatikana zikionesha ubadhirifu wa Sh zaidi ya milioni 763 katika halmashauri.

Yah: Tanzania na maendeleo ya mdomo

Nianze kwa kuwashukuru sana wazazi wangu walionikanya wakati naoa kwamba maisha ya ndoa ni kama glasi ndani ya kabati, ipo siku lazima kabati litayumba na glasi zitagongana, na ikitokea hivyo katika maisha yangu ya ndoa lazima nitumie kuta nne za chumbani kwangu kumaliza kelele zetu za glasi, ugomvi na sintofahamu yoyote ile.

Mkombozi wako kiuchumi ni wewe

 

Wiki iliyopita niliandika makala kuhusu fikra zinavyoweza kukukomboa kiuchumi. Katika makala yale nilieleza kuwa ili kufanikiwa kibiashara na kiajira tunahitaji hamasa kuliko hata kubadilisha siasa zinazotawala na Katiba mpya. Nilisema mtu namba moja wa kuukomboa uchumi wako ni wewe mwenyewe.

 

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Hatuwezi kuthibitisha wanaotusaidia

“Tunatambua kuna uwezekano kwamba hao wanaotusaidia wanaweza kuwa na nia tofauti. Hivi ndivyo tunaambiwa na hatuna uthibitisho kwamba haiko hivyo. Lakini tuna ushahidi wa mahitaji yetu na misaada ya vitendo.

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Alizaliwa Aprili 13, 1922 kijijini Butiama, Mara. Alifariki Oktoba 14, 1999 nchini Uingereza.

Ustawi wako kiuchumi unategemea fikra yako

 

 

Watanzania (na wanadamu wengine duniani kote) nyakati hizi; tunaishi kwenye zama zenye misongo mikubwa ya kimaisha; kubwa likiwa ni tatizo la kiuchumi.

Utajiri wa Loliondo na laana yake (Hitimisho)

Sehemu iliyopita, Mwandishi Wetu alieleza Kamati iliyoundwa na CCM kuchunguza mgogoro wa Loliondo. Sehemu hii ya nne na ya mwisho, anaeleza ubatili wa Kamati ya Nchemba. Endelea…