JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

FASIHI FASAHA

Ombaomba ni unyonge wa Mwafrika

“Unyonge wetu ni wa aina mbili, unyonge wa kwanza ulio mkubwa zaidi ni unyonge wa moyo; unyonge wa roho. Unyonge wa pili ndiyo huu wa umaskini wa kukosa chochote. Ni kweli hatuna chochote, hatuna nguvu.” Haya ni maneno ya Mwalimu Nyerere alipowahutubia walimu katika Sherehe za Vijana kwenye  Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, Mei 30, 1969.

Obama ampandisha chati Lowassa

Hatua ya Rais wa Marekani, Barack Obama, kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Symbion Ubungo jijini Dar es Salaam, imeamsha mjadala mzito katika jamii uliowafanya Watanzania kuanza kumhurumia Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, wakiona alionewa.

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Mahitaji ya wananchi yalindwe

“Lazima tuendelee kuhakikisha kwamba mahitaji ya msingi ya watu wote yanapatikana na yanalindwa. Lengo letu lazima liendelee kuwa kuinua hali ya maisha ya kila mtu, na kila mtu aweze kupata huduma za msingi za elimu na matibabu.”

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Hoja ni kutii sheria, si kufuta kauli

Hivi karibuni niliandika makala nikizungumzia kauli za wanasiasa na athari zake kwa umma. Nilizungumza kuhusu kauli zinazochochea vurugu, migongano na kuleta chuki na uvunjifu wa amani.

Mandela alifunguliwa milango ya gereza, akagoma kutoka

Ikiwa Mungu atapenda, maana hadi tunachapisha makala haya, Mzee wetu, mwana wa kweli wa Afrika, Nelson Rolihlahla Mandela maarufu kama Madiba, wa Afrika ya Kusini, Alhamisi wiki hii atatimizi miaka 95 ya kuzaliwa. Mandela anaumwa akisumbuliwa na ugonjwa wa maambukizi ya mapafu na amelazwa katika hospitali moja jijini Pretoria, nchini humo.

Utajiri wa Loliondo na laana yake (2)

 

Mfululizo huu wa makala kuhusu Loliondo ulianza wiki mbili zilizopita. Kwenye toleo la mwisho, tuliishia kwenye kipengele kinachopingana na propaganda za uongo kwamba Serikali imechukua ardhi ya vijiji. Mwandishi anasema baadhi ya madiwani na NGOs zimetumiwa kueneza uongo huo kwa maslahi yao ya kisiasa na kiuchumi. Endelea.