Kiwanda cha Bora Kimeteketea Kwa Moto Usiku wa Jana

KIWANDA cha kutengeneza viatu cha Bora kinachotengeneza viatu aina ya kandambili kinateketea kwa moto usiku huu chanzo cha moto chake hakijafahamika wala madhara yaliyosababishwa na moto huo.

Moto ni mkubwa sana ndani ya kiwanda hicho na kikosi cha zima moto kimeishiwa maji.

Hatibu Rashidi  ambaye ni Operation Manager wa Nile Security wanaojihusisha na ulinzi ndani ya kiwanda amesema moto ulianza mida ya saa mbili usiku.