Na Mussa Augustine,JamhuriMedia

Ikiwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imejipambanua kuboresha mazingira ya uwekezaji,wawekezaji Wazawa wamekua wakiunga Mkono jitihada za Serikali katika shughuli za maendeleo.

Kufuatia hatua hiyo Kampuni ya Wazawa ya RECO Engineering Co Limited ni mshirika wa kuaminika katika kutoa huduma za kiuhandisi kwa makampuni na karakana kadhaa za kiuhandisi nchini Tanzania tangu mwaka tangu 1948.

Hii ni sehemu ambayo inayeyusha chuma ili kiwe kimiminika.

Akizungumza na mwandishi wa makala haya wakati wa mahojiano maalumu Kiwandani hapo Mhandisi wa Reco Engineering Ltd Ferdinand Bihondwa anasema kwamba lengo lao kuu ni kutoa huduma mahsusi ambazo wateja wetu wanazitarajia na njia pekee ya kufanikisha hili ni kupitia uwezo wetu mkubwa kiuwekezaji na ubora wetu kwa wateja.

Anasema kuwa RECO ni kampuni yenye uzoefu inayotoa huduma kwa uaminifu na utaalamu usio na kifani huku maono yetu yakiwa kiongozi wa sekta kwa kutumia teknolojia ya kisasa zaidi na safu ya huduma za utengenezaji ambazo hutoa suluhisho kwa mradi wowote wa kiuhandisi.

Anasema bora wa bidhaa zetu kwa wateja wetu ndio lengo kuu tangu mwanzo hadi mwisho wa kumalizika kwa mradi na pia tunatoa ushauri wa kihandisi ili kuhakikisha utekelezaji wa mradi katika mchakato mzima wa uendelezaji unakidhi viwango.

Vifaa ambavyo vinatumika kupasulia miamba ambapo vinatengenezwa na kampuni ya RECO Engineering

“Lakini pia unapofanya kazi na Reco Engineering Co Ltd utapokea bidhaa ya ubora wa hali ya juu kwa bei ya ushindani kutokana na kwamba tunazalisha wenyewe kupitia kampuni yetu” anasema Mhandisi Bihondwa

Anaendelea kufafanua kiwa kampuni ya RECO Engineering Limited yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam, Tanzania ni mabingwa wa upandaji wa chrome ngumu kwa njia ya umeme, mchakato wa upandaji wa chrome ngumu huongeza sifa za kimitambo na kimwili za componets zote pamoja na barabara, kipenyo cha bomba la ndani, rolls na pini.

Anasema timu yetu ya hard chroming ina uzoefu wa miaka 10 katika uwanja huu na imefanya miradi mingi ya sekta mbalimbali za viwanda kama vile Usafiri wa Anga, viwanda vya baharini, viwanda vya chuma, viwanda vya kutengeneza nguo za viwandani na vinginevyo,(OEMS) na kwa ajili ya ukarabati wa vipengele vya silinda.

Vipengele vya Kupanda Chrome ngumu Kuzuia oxidation ya fomu Msuguano wa chini Sugu ya abrasion Ugumu wa uso inastahimili kutu Mali ya paramagnetic

Mhandisi Ferdinand Bihondwa akielezea namna vipuli vya kuvunjia miamba vinavyotengenezwa na kampuni hiyo

Huduma zetu

Kuhusu huduma wanazotoa mhandisi Bihondwa anasema RECO Engineering Ltd inatoa huduma za kuuchomelea, kukarabati, upandaji wa shaba, ukingo wa mikono, usahihi hufanya kazi chrome, Kupanda kwa Chrome ngumu, Kusaga, Usafishaji Mzuri na Idara yetu ya Foundry inafuata viwango vya kimataifa vya uwasilishaji ili kukidhi matarajio ya wateja.

Anasema kuwa idara ya Uhandisi ina wataalamu walio na uzoefu wa zaidi ya miaka 20 na Kitengo hiki kina uwezo wa kutengeneza Picha ya Grey, Chuma cha Ductile, Chuma cha pua, Chuma cha pua cha Duplex na aloi nyingine bora kwa Vipimo vya Kimataifa.

Hii ni sehemu ambayo inayeyusha chuma ili kiwe kimiminika.

Udhibiti wa Ubora

Mhandisi Bihondwa anafafanua kuwa kuna mashine ya Spectro ya Utungaji wa Kemikali yenye (Nguvu za Metal) zaidi ya vipengele 26 ambayo inasaidia kudhibiti ubora wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo.

Anasema wanafanya aribio la gla maabara ya mchanga kamili ,Upimaji wa ugumu, Kinasa cha chati cha Kinasa cha Matibabu ya Joto Kiotomatiki,Jedwali la uso kwa ajili ya kukagua kipenyo, kipimo cha ukungu na msingi wa ugumu.

Anasema kitengo chao cha uhandisi wa mitambo kinatumia mashine ambazo huchonga kwa ukamilifu kabisa na ubora usio kifani mashine hizi zinalingana na viwango vya ubora wa kimataifa na hivyo kutusaidia kupata wateja wengi Tanzania nzima.

“Moja ya mashine chache za hali ya juu ambazo kutumia kutekeleza huduma zetu katika kitengo hiki ni pamoja na Mashine ya Gear Hobber, Mashine ya Lathe, verticles Lathe Machine na mashine ya kusaga” anasema Mhandisi Bihondwa.

Anaendelea kueleza kiwa katika kitengo chao cha magari hutumia mashine za kisasa kutoa usahihi kabisa na machines kuendana na sehemu za magari zenye ubora wa kimataifa na mashine hizi zinalingana na viwango vya ubora wa kimataifa na hivyo kutusaidia kupata wateja wengi.

Anasema wanatoa usikivu wa kibinafsi kwa mahitaji maalum ya wateja wao, sisi ni kipaumbele cha mtu binafsi kwa mahitaji maalum ya wateja wetu tunajivunia sifa yetu kwa kujitolea kwa huduma bora, na taaluma.

Anasema tumetumia mwaka kujenga timu ya kirafiki, yenye manufaa na yenye ufanisi ambayo hufanya chochote kinachohitajika ili kutimiza mahitaji ya mteja wetu.

Reco Engineering Company Ltd tunatoa huduma za kihandisi kwa makampuni mbalimbali na karakana za Tanzania tangu 1948 Kama tulivyosema awali.

Anasema lengo ni kutoa utendaji na huduma ya kipekee ambayo wateja wao wanatarajia kufanikisha hili kupitia nguvu ya mchakato wao wa uwekezaji na ubora wa watu wao kutoka kwa operesheni ya watu watano hadi duka la mashine lililo na vifaa kamili na wafanyikazi 50.

“Wafanyakazi wetu wana uzoefu, kuanzia miaka 20 hadi 30 katika fani ya uhandisi kama tulivyosema hapo mwanzo juu ya ufanisi wa kampuni hii hivyo mafundi wetu, wasimamizi, wahandisi na wasimamizi wamejitolea, wamefunzwa sana na vifaa vyetu vya usahihi viko juu kwa ubora” anasema.

Fadhiri Furaha ni mtalaamu kitengo cha uyeyushaji chuma katika kampuni ya Reco Engineering akizungumza kitaalamu anasema kuwa kitengo chake kifanya kazi ya kutengeneza chuma kwa aina nne zenye matumuzi tofauti

Anasema kuwa aina ya kwanza ya chuma ni Manganizi ambayo inatumika kulinda chombo kinachotumika kupasulia miamba na aina nyingine haikromu ambayo inatumika kuvunja miamba na sitiri inatumika kutengeneza bidhaa tofauti kama vile jembe,panga, na aina ya mwisho ni kifaa kinachotumika kutengeneza mifuniko ya baràbarani, ambayo inatumika kufunika chemba mbalimbali.

Naye mtaalamu wa mitambo Machenical Engneeringa Matheo Mbumila akizungumzia kitengo chake anasema kuwa yeye ameaza kazi mwaka 1995 na anauzoefu mkubwa na kwenye kitengo chake wanafanya kazi za kuchonga vyuma vya aina mbalimbali kama shafuti.selinder Add.nk

Anasema kuwa wakati anakuja hapo kulikuwa hakuna sehemu ya kuyeyusha chuma lakini sasa hivi kuna sehemu ya kuyeyusha chuma ambapo wateja kutoka nchi za Afrika Masharika ikiwamo Uganga ,Kenya , wote wanakuja kutaka huduma na wanakuja kufanya kazi.

“Kwakweli hivi sasa kuna mafanikio makubwa kwani watu wanakuna wanamimina chuma ,makasha yote ya lugoba wanaleta hapa kwetu ili kuifanyizia kazi na idara yetu ni uchongaji, yaani (Mashine shop) .

Hata hivyo Mhandisi wa kampuni hiyo Ferdnand Bihongwa anawashauri watanzania kujenga utamaduni wa kupenda kutumia vipuli vinavyozalishwa hapa nchini hasa kutoka kampuni ya Reco Engineering kwani bidhaa zinazozalishwa kwenye kampuni hiyo zina ubora unaokidhi viwango.

Mhandisi Bihondwa anasema kuwa kampuni ya Reco kimsingi ilianzishwa mwaka 1948 kwa ajili ya kuunda aina mbalimbali za vipuli na ku repair viungo vya engine kwa ajili ya vyombo vya moto.

Anasema kuwa kampuni hiyo ambayo iliyoazishwa kwa lengo la kuunda vipuli mbalimbali vikiwamo vilivyo kwisha tumika na kufufua aina mbalimbali za mashine ambazo zimekufa na zingine zilizokuwa zimechakaa hivyo wao kama Reco wanazirudisha kwenye ubora kwa ajili ya matumizi tena.

Anaongeza kuwa kutokana na kukua kwa teknolojia watu wengi wamekuwa wakiagiza mashine mbalimbali kutoka nje ya nchi hali ambayo inazolotesha biashara kwasababu ya kununua mashine ambazo zimetumika.

Anasema kuwa baada ya kuona changamoto ya uhitaji wa mashine kutoka nje wao kama Reco walikuja na mbinu mpya ya kuyeyusha chuma na baada ya kuyeyusha chuma unapata kitu ambacho kipo katika mfumo wa kimiminika.

‘’Kama unakumbuka zamani ili utoe maji machafu tulikuwa hatuna mabomba ya plastiki ya kutolea maji taka tulikuwa tunatumia mabomba magumu cast iron pipes ambayo yalikuwa yanatokana na kuyeyushwa kwenye majiko hivyo kwa sasa teknolojia tumehamisha huku.

Anafafanua kuwa hivi sasa wamekwenda mbali zaidi wanazuia kutu kwa kutumia teknolojia mpya ambayo wanayo kama chroming na galvanising hivyo wanajaribu kuwapa wateja kitu kilicho bora na kinacho zalishwa na Reco Engineering.

Anasema kuwa RECO wamekwenda mbali zaidi kwa kuanza kutengeneza mifuniko inayotumika kwenye chemba za barabarani pamoja na kwenye mitaro ya maji ,majumbani na viwandani na hiyo ni kuendana na kasi ya teknolojia kama dunia inavyotaka.

Mbali na hayo RECO Engineering inahudumia teknolojia ya Casting katika baadhi ya nchi barani Afrika ambapo hawana hiyo teknolojia,na nchi hizo ni Rwanda,Malawi,Zambia na Msumbiji.

“Baadhi ya kampuni tunazofanya nazo kazi ni Yapi Merkezi Insaat,Tanga Cement Company limited,Tanzania International Container (TICTS) ,Toyota Tanzania Ltd,Tanzania Printing Services Ltd,Sao Hill Industries Limited,Ramani Investment Ltd na Mbeya Quarry Associates T.Ltd.

By Jamhuri