Jeetu Patel awawekea ngumu METL
Mfanyabiashara maarufu wa jijini Dar es Salaam, Jeetu Patel, wakati mgogoro huu unaendelea yeye ndiye aliyekuwa mpangaji katika kiwanja Na 10 kupitia kampuni yake ya Noble Azania Investment (NAIL). Kampuni hii ilipinga wazo lililokuwa limetolewa kuwa sehemu ya kiwanja Na 10 imegwe na kumtengenezea barabara METL. Ilifungua kesi mahakamani na kupewa hati ya zuio.

Kuona hivyo, METL iliamua kununua kiwanja hicho Na 10 kwa Sh bilioni 2.046 na akasubiri kampuni ya Jeetu Patel imalize muda wake wa upangaji afanye marekebisho atakayo. Ikumbukwe kiwanja hiki kilikuwa mali ya TANGOLD, kampuni ya kuchonga madini iliyoishia kuvunjwa kwa aibu kubwa, ila mitambo yake iliendelea kubaki kwenye kiwanja hicho.

By Jamhuri