IGP Sirro usitishe wakosoaji, safisha Polisi
Nimesikiliza kauli ya Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro, kuhusu kupatikana kwa Mo Dewji. IGP Sirro amesema pamoja na mengi mengine kwamba wanaotafuta uadui na Jeshi la Polisi wasije wakalaumu litakapowatokea la kutokea. Kwake yeye, kukosoa utendaji wa Jeshi la Polisi katika masuala makubwa kama utekaji nyara wa raia ni kukosa uzalendo. Amehoji uraia wetu…