Rais Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ) lijikite kwenye kutumia mbinu za kisayansi na teknolojia katika kazi zao ili kudumisha ulinzi na usalama.

Rais Samia ameyasema hayo alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa Saba wa CDF na Makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wa mwaka 2023 , uliyofanyika katika kambi ya JWTZ 302 KV Lugalo, jijini Dar es Salaam, tarehe 22 Januari 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda wakati wa mkutano wa CDF na Makamanda kwa mwaka 2023 ambao ulifanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi, Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Maafisa Majenerali mbalimbali wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stergomena Tax mara baada ya kuwasili Lugalo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufungua mkutano wa CDF na Makamanda kwa mwaka 2023, tarehe 22 Januari, 2024.
Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Maafisa Majenerali mbalimbali wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wakiwa kwenye Mkutano wa CDF na Makamanda uliofanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania (CDF) Jenerali Jacob John Mkunda kabla ya kufungua mkutano wa Makamanda kwa mwaka 2023 uliofanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.
Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Maafisa Majenerali mbalimbali wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wakiimba Wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa mkutano wa CDF na Makamanda uliofanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.