Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali wakati akifunga Mafunzo ya Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha kwa Mfipa mkoani Pwani tarehe 27 Agosti, 2023.
Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa wakisikiliza kwa makini hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akifunga Mafunzo yao yaliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha kwa Mfipa Mkoani Pwani tarehe 27 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha kwa Mfipa Mkoani Pwani tarehe 27 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha kwa Mfipa Mkoani Pwani kwa ajili ya kufunga Mafunzo ya Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa tarehe 27 Agosti, 2023.