Simba yatinga hatua ya makundi Ligi Mabingwa Afrika

Klabu ya Simba imefanikiwa kutinga hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuichapa timu ya Primeiro de Agosto ya nchini Angola 1-0 na kuwa jumla ya mabao 4-1 baada ya mechi ya kwanza Simba Sc kushinda 3-1 ugenini.

Mechi hiyo ambayo imepigwa katika dimba la Benjamini Mkapa, Simba Sc imefanikiwa kutawala mchezo na kuwafanya mashabiki ambao waliujaza uwanja kufurahia kandanda safi kutoka kwa mastaa wa timu hiyo.

Ni Moses Phiri ambaye amekuwa moto katika mechi za hii karibu amepachika bao safi ambalo liliwafanya Simba Sc kuwahakikishia kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.