Wajumbe katika mkutano  wa Uongozi wa Bara la Afrika wamezitaka nchi za Afrika kujenga mfumo imara wa ugavi wa thamani kwa kilimo kwa sababu sekta hiyo inatoa fursa bora ya kuongezeka kwa biashara ndani ya Afrika.

Viongozi na washiriki wengine walibainisha kuwa Afrika ina ardhi ya kutosha kwa kilimo ambayo inaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji na maendeleo ya bara hilo, ikishikilia zaidi ya nusu ya ardhi ya kilimo duniani na rasilimali kubwa za maji zenye uwezo wa kutosha kwa umwagiliaji.

Zaidi ya hayo, kwa idadi ya watu inayokadiriwa kuwa bilioni 1.3 ambapo wengi wao (angalau asilimia 70) wanaishi vijijini na wanajishughulisha na kilimo kama shughuli yao kuu ya kiuchumi inaonekana kuwa ni jambo la kushangaza kwamba bara hilo bado linachangia asilimia 4 tu ya uzalishaji wa kilimo ulimwenguni pote, walibainisha.

Akizungumza katika Mkutano huo wa Uongozi wa Afrika (ALF) ambao ulianza hapo Alhamisi, Rais Mstaafu wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete alibainisha kuwa sekta hiyo ilichangia sehemu kubwa ya Pato la Taifa na mapato ya fedha za kigeni kwa bara hilo na hivyo kutoa fursa ya kipekee kwa biashara ya ndani ya Afrika inayohitajika sana.

“Hakuna sekta inayowaajiri watu wengi kama kilimo, lakini bado haijafikia uwezo wake kamili, kwa hiyo kujadili jinsi ya kufungua uwezo wake ni jambo sahihi kufanya. Zaidi inahitajika kufanywa katika nchi za Afrika na kuunganisha na jinsi ya kuondoa umasikini, kuondoa upungufu wa chakula na njaa. Hii ni fursa kubwa kwa ushirikiano katika mnyororo wa biashara ya ndani ya Afrika,”alisema.

Taasisi ya UONGOZI imeandaa Mkutano wa 7 wa ALF mwaka huu kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA) kwa kauli mbiu “Kukuza biashara ndani ya Afrika ili kufungua uwezo wa kulimo barani Afrika.

“Kama Mwenyeji na Mlezi wa ALF, Dkt. Kikwete, alibainisha kwamba kilimo ni nguzo kuu ya watu wengi katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na utinwa mgongo wa uchumi, hakuna mahali bora pa kuanza katika kipaumbele cha kuzingatia na uvumbuzi ikiwa bara linataka kuongeza biashara kati yao,” alisisitiza.

Alisema sekta hii muhimu haijafanikiwa kufanya kazi kikamilifu kwasababu ya vizuizi vingi vinavyozuia utumiaji kamili wa uwezo wake. Kwahivyo, kwa Jukwaa hili kujadili kufungua uwezo wa kilimo barani Afrika ni jambo sahihi kufanya.

Dkt. Kikwete alikiri kuwa juhudi zinafanywa na Serikali za Afrika kwa ajili ya wakulima wadogo wa Kiafrika na wadau wengine ili kubadilisha hali ya kilimo barani Afrika na kwamba tayari kuna maendeleo makubwa yaliyofikiwa na mafanikio mengi yamepatikana.

“Hata hivyo, kuna mengi zaidi yanahitajika kufanywa ili kilimo kiweze kuchangia kikamilifu katika ukuaji na maendeleo ya mataifa ya Afrika na ustawi na utajiri wa watu wa Afrika,” alisema.

“Mpaka sasa mambo yamekwenda vizuri lakini bado hayatoshi kama inavyothibitishwa na kiwango cha umasikini katika maeneo mengi ya vijijini ambap watu wetu wengi wanaishi na ripoti zisizoisha za watu kusumbuliwa na ukosefu wa chakula na njaa barani Afrika.” alisema.

Alikuwa na mtazamo kwamba ripti za Afrika kuwa bado inatumia kiasi kikubwa cha fedha za kigeni kununua chakula hazifurahishi kusikia. Vilevile, aliongeza kwamba ripoti za Afrika kuwa bado inauza malighafi za kilimo kwa nchi zilizoendelea na kununua bidhaa zilizotengenezwa kutokana na malighafi hizo ambazo Afrika ilizipeleka nje hazifurahishi.

“Uwekezaji katika watu wetu hasa wakulima wadogo na vijana wetu; uwekezaji katika taasisi na miundombinu yetu ili kuhakikisha mazingira mazuri ya kufanya biashara yanahitajika; na zaidi ya yote kujitolea kwetu kuwekeza katika ajenda ya muda mrefu ya Afrika kuliko vipaumbele vya ndani vya muda mfupi.

Mlezi wa Africa Leaders Forum Rais mstaafu Dkt Jakaya Kikwete akihutubia mkutano huo ,Accra,Ghana Alhamis.Viongozi wengine wa Kiafrika waliohudhuria ni pamoja na Rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, Rais wa zamani wa Tunisia Dr. Mohamed Moncef Marzouki, Rais wa zamani wa Nigeria Dr Goodluck Ebele Jonathan, Rais wa zamani wa Benin, Thomas Boni Yayi, Rais wa zamani wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf, Waziri Mkuu wa zamani wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn Boshe, na Rais wa zamani wa Sierra Leone Dr. Ernest Bai Koroma.Picha na Imani Nsamila

“Akifungua Mkutano mapema Rais wa Ghana, Nana Addo Dankwa Akufo-Addo, alisema biashara ndani ya Afrika ni moja ya chini kabisa katika eneo hilo na bado imegawanyika na uwezo mdogo wa uzalishaji.

“Kuna nguvu katika umoja. Ikiwa nchi zote 54 zenye watu bilioni 1.3 na Pato la Taifa la dola trilioni 3 zitashirikiana, hii ni fursa kubwa ya ukuaji na kukabiliana na ongezeko la bei na kutokuwa na uhakika wa kimataifa.” alisema.

Alisema kuwa kwa kuwa hii inatoa fursa sekta binafsi, serikali lazima iwe na ujasiri kupitia hatua zenye mkakati wa kujenga thamani na lengo kubwa zaidi.

Katibu Mkuu wa AfCFTA, Wamkele Mene, pia alibainisha kuwa Afrika bado ni bara linalonunua chakula kutoka nje kwa kiwango kikubwa, na gharama ya kununua chakula kutoka nje ilifika dola bilioni 80 kati ya mwaka 2015 na 2017.

“Tunahitaji kufungua uwezo wa jamii zetu za vijijini ili kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani wa kimataifa na kuwezesha wakulima wadogo kuwa sehemu ya biashara ya kimataifa. Kwa kutambua jukumu la sekta binafsi na biashara zinazomilikiwa na wanawake, AfCFTA imetoa kipaumbele kwa kilimo na usindikaji.” alisema

Akitoa muktadha wa kikao cha jumla, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekele alisema soko la kilimo la Afrika bado limegawanyika na kusambaa, ambayo inafanya hali ya ujumuishaji kama njia ya kuongeza soko na kufanya bara kuwa mchezaji wa kimataifa.

Aliomba taasisi za kifedha kushirikiana katika soko kama sehemu ya suluhisho la kupata fedha za kusaidia mifumo ya kilimo barani Afrika. 

Viongozi wengine wa Kiafrika waliohudhuria ni pamoja na Rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, Rais wa zamani wa Tunisia Dr. Mohamed Moncef Marzouki, Rais wa zamani wa Nigeria Dr Goodluck Ebele Jonathan, Rais wa zamani wa Benin, Thomas Boni Yayi, Rais wa zamani wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf, Waziri Mkuu wa zamani wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn Boshe, na Rais wa zamani wa Sierra Leone Dr. Ernest Bai Koroma.

Pia walihudhuria  sekta binafsi kutoka kote barani Afrika, wakitafuta kutoa nafasi ya kushiriki uzoefu na ufahamu wao katika kufanikisha biashara ya kilimo kati ya nchi za Afrika. Kupitia kipindi cha ukimya na kikao cha kuonyesha video zake zenye nguvu kuhusu mageuzi ya Afrika, wajumbe walitoa heshima fupi kwa Mpatanishi wa ALF na Rais wa zamani Benjamin Mkapa.

Tukio hili la siku 2 limeangazia uwezo wa kilimo barani Afrika na fursa zinazojitokeza kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, kushiriki uzoefu na masomo kuhusu vikwazo (ndani na kimataifa) katika kufikia uwezo wa kilimo barani Afrika, kujadili uwezo na vikwazo, pamoja na mahitaji halisi na ya vitendo ya kutekeleza AfCFTA ndani ya muktadha wa kilimo barani Afrika na kutambua vipaumbele na ramani ya barabara kwa utekelezaji wa mtazamo wa biashara ya kilimo chini ya AfCFTA ili kufikia lengo lake la kiuchumi la kubadilisha.

Wadhamini wa tukio walikuwa ni AfCFTA, Benki ya NMB, Benki ya CRDB, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, NBC Bank Tanzania, ASAS CommNet na RAHISI, DTB Tanzania, Karibu Travel, Jarida la Uongozi wa Kiafrika na wengine kadhaa.

By Jamhuri