Skip to main content
JAMHURI MEDIA
Tunaanzia wanapoishia wengine
Home
Kitaifa
Biashara
Siasa
Uchumi
Kimataifa
Makala
Siasa
Uchumi
MCHANGANYIKO
Michezo
Burudani
Kazi/Ajira
Gazeti La Jamhuri
Sitanii
JAMHURI YA WAUNGWANA
Nyundo ya Wiki
Search
November 7, 2022
Habari Mpya
Bunge la Afrika laombeleza vifo vya watu 19 ajali ya ndege
Jamhuri
Comments Off
on Bunge la Afrika laombeleza vifo vya watu 19 ajali ya ndege
Wabunge wa Bunge la Afrika (PAP) wakiwa wamesimama kwa dakika moja kuwakumbuka Watanzania waliofariki dunia kwenye ajali ya ndege ya Kampuni ya Precision Air iliyotokea nchini Tanzania Jumapili Novemba 6,2022 katika Ziwa Victoria baada ya kushindwa kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba mkoani Kagera. Picha na Kadama Malunde – Midrand Afrika Kusini
Rais wa Bunge la Afrika (Pan African Parliament – PAP), Mhe. Chifu Fortune Charumbira akiongoza Mkutano wa Bunge la Afrika leo Jumatatu Novemba 7,2022
Rais wa Bunge la Afrika (Pan African Parliament – PAP), Mhe. Chifu Fortune Charumbira (kushoto) akimpa pole Mbunge wa Bunge la Afrika kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anatropia Theonest kwa niaba ya Serikali ya Tanzania kufuatia ajali ya ndege ya Kampuni ya Precision Air iliyoua watu 19 baada ya kuanguka katika Ziwa Victoria Nchini Tanzania
Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wote wametuma salamu zao za faraja kwa familia za waathirika wa ajali hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila ametaja marehemu kuwa ni pamoja na Neema Faraja, Hanifa Hamza, Aneth Kaaya, Victoria Laurean, Said Malat Lyangana, Iman Paul, Faraji Yusuph, na Lin Zhang.
Wengine ni Sauli Epimark, Zacharia Mlacha, Eunice Ndirangu, Mtani Njegere, Zaituni Shillah, Dk Alice Simwinga na afisa wa kwanza wa ndege hiyo, Peter Odhiambo.
Hakuna miili mingine iliyopatikana. Taarifa za awali zilieleza kuwa ajali hiyo ilitokana na hali mbaya ya hewa. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesitisha shughuli zote za ndege katika uwanja wa ndege wa Bukoba kwa muda usiojulikana.
Shirika la ndege la AirTanzania, pia limesitisha safari zake Jumapili kuelekea Bukoba.
Timu ya wataalamu kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwa sasa ipo mjini Bukoba kuchunguza tukio hilo
Post Views:
247
Previous Post
Ugonjwa wa figo unavyogharimu maisha
Next Post
Kijana aliyeokoa watu ajali ya ndege Serikali 'yamuheshimisha'
Mbetto :Jussa acha matamshi ya kibaguzi Zanzibar
Dereva aliyesababisha ajali iliyoua watu nane akamatwa
WHI yatunukiwa tuzo ya nyumba za gharama nafuu zaidi Afrika
NEEC yadhamiria kuwainua kiuchumi wananchi kwa kutoa elimu ya kutambua fursa
Setilaiti iliyotengenezwa na Boeing yavunjika angani
Habari mpya
Mbetto :Jussa acha matamshi ya kibaguzi Zanzibar
Dereva aliyesababisha ajali iliyoua watu nane akamatwa
WHI yatunukiwa tuzo ya nyumba za gharama nafuu zaidi Afrika
NEEC yadhamiria kuwainua kiuchumi wananchi kwa kutoa elimu ya kutambua fursa
Setilaiti iliyotengenezwa na Boeing yavunjika angani
Geita yaupokea mradi wa bilioni 17 kusambaza umeme kwenye vitongoji 105
Kongamano la ARGe0-C10 kuongeza kasi uendelezaji jotoardhi Afrika Dk Mataragio
Urusi yafanya mashambulizi usiku kucha mjini Kyiv Ukraine
Profesa Mkumbo avutiwa na utendaji wa bandari ya Dar
FCS, LATRA CCC wasaini makubaliano kuimarisha ulinzi na haki ya walaji sekta ya usafiri ardhini
Mfumo wa PAIS kudhibiti migogoro baina wanyamapori na binadamu Babati
Waziri Bashungwa aongoza utiaji saini ujenzi wa daraja la Jangwani
GST kukamilisha upatikanaji wa ithibati vyungu kuyeyushia sampuli za dhahabu
Kamati ya Bunge yaridhishwa utendajikazi Wizara ya Nishati
Shule za Mbeya kufanyiwa ukarabati mkubwa, zitoe mazingira bora ya kujifunzia