Maandamano ya upinzani yameanza nchini Kenya, licha ya kutangazwa na polisi kuwa haramu, na kusababisha matumizi ya vitoa machozi na vyombo vya sheria kuwatawanya waandamanaji katika miji mbalimbali.

Inspekta Jenerali wa Polisi alisema kuwa “mamlaka hawana lingine ila kuchukua hatua zinazohitajika kutawanya maandamano hayo haramu”, kama ilivyotajwa katika taarifa aliyoitoa Jumanne jioni.

Barabara kuu za Nairobi, Kisii, Kisumu na Nyeri zina msongamano mdogo, na video za mtandaoni zinaonyesha barabara zilizofungwa katika maeneo kadhaa. Biashara nyingi zimesalia kufungwa, na usafiri umesimama.

Ijumaa iliyopita, makabiliano kati ya waandamanaji wa upinzani na polisi yalisababisha vifo vya watu sita katika miji mingi.

Wahudumu wa magari ya utumishi wa umma katika miji kadhaa wamejiunga na maandamano hayo, na kusitisha shughuli zao kupinga kupanda kwa gharama ya mafuta.

Madereva wa programu zinazotumia njia za kidijitali pia wamejiunga na maandamano, wakielezea wasiwasi wao kuhusu gharama za mafuta, ukosefu wa marekebisho ya bei na masuala ya usalama.

Waandalizi hao wanahimiza ushiriki mkubwa kote nchini Kenya, wakitaka kufutwa kwa sheria mpya ya fedha inayoongeza ushuru wa mafuta maradufu na kuweka ushuru wa nyumba wa 1.5% kwa wafanyikazi.

Rais wa Kenya, William Ruto, anatetea sheria ya fedha iliyositishwa kwa muda, akisema kuwa itashughulikia masuala ya ulipaji wa madeni na kuunda nafasi za kazi kwa vijana wasio na ajira.

Anashutumu upinzani kwa kuhujumu mustakabali wa mamilioni ya vijana wasio na ajira na kuapa kuzuia kupoteza maisha kutokana na maandamano.

Mahakama kuu jijini Nairobi imesitisha utekelezwaji wa sheria ya fedha, ikitaja wasiwasi mkubwa wa kikatiba.

By Jamhuri