Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Ukumbi wa Kikwete kwa ajili ya Kufutarisha Viongozi pamoja na Makundi mbalimbali, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Mama Janeth Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Omar
Viongozi mbalimbali, Wasanii, Wahariri wa vyombo vya Habari pamoja na Wageni wengine wakiwa kwenye ukumbi wa Kikwete kwa ajili ya Futari Ikulu Jijini Dar es Salaam. Futari hiyo iliandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan tarehe 15 Aprili 2023.

By Jamhuri