…………………………………………………………..

Timu za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),mabingwa watetezi kwa upande wa mpira wa miguu na Hospitali ya Rufaa KCMC ya Kilimanjaro zimetoshana nguvu baada ya kufungana bao 1-1, katika michuano ya Shimuta inayoendelea Jijini Tanga.

Mchezo huo ambao umefanyika kwenye viwanja vya mizani Jijini Tanga ulikuwa na upinzani mkubwa kwa kila timu kutaka kupata matokeo mazuri jambo ambalo lilizidisha ugumu wa mchezo huo

Timu ya KCMC ndio walikuwa wa kwanza kupata bao la kupitia Yusuph Madili aliyepiga faulu ya kona iliyotinga moja kwa moja na hivyo kuamsha shangwe na hari kwa mashabiki wao.

Mpaka timu hizo zinakwenda mapumziko KCMC walikuwa mbele kwa bao 1-0 ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi kutokana na kila timu kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake na kuingiza nguvu mpya.

Walionekana kujipanga na kujiimarisha katika kipindi hicho timu ya TRA ilianzisha mashambulizi mfululizo lango mwa wapinzani wao huku wakicheza pasi fupi fupi na ndefu .

Kutokana na aina hiyo ya mchezo ambao walikuwa wakicheza iliwapelekea kuweza kupata bao la kusawadhisha kupitia kwa Datram Benzema ambaye alitumia uzembe wa mabeki kupachika wavuni bao hilo na hivyo kuamsha shangwe uwanja mzima.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo Katibu wa timu ya TRA Kamna Shomari alisema kwamba wanamshukuru mwenyezi Mungu kwa kuwawezesha kupata Sare na wana mechi nyengine.

Alisema kwamba hivyo wana matumaini watarekebisha mapungufu na kufanya vizuri Michezo ijayo na kwamba wamepania kuhakikisha wanapata matokeo mazuri kwenye mechi yao.

By Jamhuri