Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu,Wizara ya Maji (wa nne kushoto) akikata utepe kuzindua Wiki ya Maji,akimwakilisha Waziri wa Maji,Mhe. Jumaa Hamidu Aweso. Uzinduzi wa Wiki ya Maji umefanyika katika Jengo jipya la Wizara ya Maji Mtumba Mjini Dodoma Leo Machi 16,2024 uliyoambatana na Matembezi kwa afya katika Mji wa Serikali Mtumba. (Picha na Mpigapicha Wetu)
Watumishi wa Sekta ya Maji wakishiriki Matembezi ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa Wiki ya Maji leo machi 16,2024 katika Mji wa Serikali Mtumba. (Picha na Mpigapicha Wetu)
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Wizara ya Maji, Wanyenda Kutta (watatu kushoto) akiongoza matembezi kwa watumishi wa Wizara ya Maji pamoja na Taasisi zake, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Wakala Wa Maji Na Usafi Wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Mfuko wa Maji Taifa wa Maji na wadau wa sekta ya maji wakati wa matembezi na uzinduzi wa Wiki ya Maji katika jingo jipya la Wizara Mtumba jijini Dodoma leo Machi 16, 2024. (Picha na Mpigapicha Wetu)

By Jamhuri