Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Dodoma

Baada ya ukaguzi wa matengenezo ya mitambo ya umeme Kidatu mkoani Morogoro leo tarehe 1 Aprili, 2024 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko ametembelea na kukagua Kituo cha kupoza umeme cha Zuzu kilichopo jijini Dodoma.

Kituo cha kupoza Umeme cha Zuzu kilipata hitilafu kubwa baada ya Gridi ya Taifa kupata hitilafu kwenye mfumo wa kudhibiti kiwango cha maji kwenye mitambo na kusababisha mitambo kujizima kwa ghafla ili kujilinda jambo lililopelekea athari kwenye mfumo mzima wa Gridi ya Taifa na maeneo mbalimbali kukosa huduma ya umeme katika kipindi hiki cha mapumziko ya sikukuu ya Pasaka.

Dkt Biteko amewapongeza wataalamu kwa kazi kubwa ya kuendelea kufanya matengenezo ya haraka katika kituo cha kupoza Umeme cha Zuzu na maeneo yote yaliyokumbwa na kadhia hiyo kote nchini huku akisisitiza wataalamu kuendelea kukamilisha matengenezo kwa haraka ili umeme urejee maeneo yote ya nchi.

By Jamhuri