Bundi ameanza kulia ndani ya klabu ya Tottenham ya London baada ya kujikuta ikisukumwa nje ya  timu nne za juu (top 4) hadi  kuangukia nafasi ya sita.

Baada ya kupata ushindi dhidi ya klabu ya Real Madrid na ushindi wa ugenini dhidi ya  Borussia Dortmund katika mashindano ya klabu bingwa barani  Ulaya (UEFA) Tottenham imeendelea kupoteza mwelekeo kila kukicha.

 Takwimu za hivi karibuni zinaonesha tangu kuanza kwa ligi timu hiyo imepoteza alama 13 kati ya 18 ambazo ilipaswa kushinda ili kuendedeleza ushindani kama ilivyozoeleka.

Akizungumzia hali hiyo Kocha wa klabu hiyo Mauricio Pochettino amesema hali kama hiyo mara nyigi hutokea  kwa timu iliyokaa katika kiwango cha juu kwa mda mrefu.

Amesema klabu hiyo kwa mda mrefu imekuwa ikikabiliwa na majeruhi hasa katika idara ya ulinzi na idara zingine.

 “Mwanzoni tulianza vizuri kwa kupata matokeo mazuri katika mashindano mbalimbali lakini gafla hali imebadilika” amenukuliwa Pochettino.

Amesema wachezaji wanatakiwa kutulia na kuanza kurudisha ari ya ushindi waliyokuwa nayo mwanzoni mwa ligi.

Amesema mwanzoni mwa ligi timu ilikuwa na  safu imara ya ulinzi tofauti na sasa ambapo wamebaki na  wachezaji kama  Jan Vertonghen, Eric Dier na Juan Foyth huku wengine wakiwa majeruhi.

Wakati hali ikiwa hivyo ndani ya klabu hivyo wachambuzi wa soka nchini humo  wamesema tatizo lingine linalosababisha kufanya bibaya kwa timu hiyo ni  kushuka kwa  kiwango cha mchezaji kama Dele Alli siku za karibuni.

Wamesema tangu msimu uanze mchezaji huyo alionesha kiwango bora kwenye ligi ya klabu  bingwa barani Ulaya dhidi ya Real Madrid baada ya hapo amekuwa mchezaji wa kawaida.

Wametolea mfano katika mechi iliyopita dhidi ya Watford alitoka uwanjani huku akitikisa kichwa kuonyesha ishara kuwa hayuko katika kiwango kilichomfanya kutambulika duniani.

 Kama hiyo haitoshi mapema mwezi Agosti mwaka huu mchezaji Danny Rose aliponda mfumo wa ulipaji mishahara ya wachezaji klabuni hapo.

“Hii ni klabu kubwa inayopaswa kuwa thamini wachezaji wake tofauti na ilivyo sasa ambapo hakuna usawa”amesema Rose.

Matokeo ya Spurs katika michezo 8 iliyopita.

Oktoba 28

Tottenham 0-1 Man United

Novemba 1 

Tottenham 3-1Real Madrid

Novemba 5

Tottenham 1-0 Crystal Palace

Novemba 18

Tottenham 0-2 Arsenal

Novemba 21

Tottenham 2-1 Dortmund

Novemba 25

Tottenham 1-1 West Brom

Novemba 28

Tottenham 1-2 Leicester City

Desemba2

Tottenham 1-1 Watford.

 

Kwa vyovyote vile haya ni matokeo yanayoendelea kumuweka kocha wa klabu hii kubwa katika wakati mgumu tangia msimu huu uanze.

By Jamhuri