Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limepokea barua kutoka CECAFA ikiomba Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano ya Kombe la Kagame kwa ngazi ya klabu.

TFF imepokea barua hiyo leo ikiitaka Tanzania iwe mwenyeji wa michuano hiyo ambayo mara nyingi hufanyika jijini Dar es Salaam inapotokea Tanzania kwa mwenyeji.

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa TFF, Clifford Mario Ndimbo, amethibitisha shirikisho hilo kupokea barua hiyo na kuahidi kuifanyia kazi.

“Ni kweli tumepokea barua ya CECAFA ikiomba Tanzania tuwe wenyeji wa michuano ya Kagame, tutaifanyia kazi na tujajua kipi cha kufanya” amesema Ndimbo.

Michuan hiyo inayohusisha nchi za Afrika Mashariki na Kati inatarajia kuanza Juni mwaka huu.

By Jamhuri