MANCHESTER UNITED YAPINGWA NYUMBANI NA KUTUPWA NJEE YA MASHINDANO YA UEFA CHAMPION LIGI

Manchester United imetupwa njee ya Mashindano UEFA Champions League baada ya kukubali kulala kwa jumla ya mabao 2-1 ikiwa Uwanja wake wa nyumbani, Old Trafford, dhidi ya Sevilla kutoka Spain.

Mabao ya Sevilla yamefungwa na Ben Yedder katika ya 74 na 78 kipindi cha pili, huku bao la United likifungwa na Lukaku kwenye dakika ya 84.

Katika mchezo wa kwanza uliopigwa Spain, timu hizo zilenda sare ya 0-0.

Matokeo hayo sasa yanaiondosha rasmi Manchester United kwenye michuano hii na inakuwa timu ya kwanza kutoka England kutolewa mashindanoni.

 

https://youtu.be/fQ_GCbKE_6o